Close Menu
Bongoforum

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

    What's Hot

    MAJINA Walioitwa Kazini Taasisi Mbalimbali za Umma

    January 14, 2026

    NAFASI za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo

    January 14, 2026

    NAFASI za Kazi Manispaa ya Tabora

    January 14, 2026
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Home
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    BongoforumBongoforum
    • Home
    • Ajira
    • Michezo
    • Makala
    • Elimu
    Subscribe
    Bongoforum
    Home»Ajira»NAFASI 709 za Kazi Mwalimu Daraja la IIIC Hisabati (Mathematics) Utumishi
    Ajira

    NAFASI 709 za Kazi Mwalimu Daraja la IIIC Hisabati (Mathematics) Utumishi

    BongoforumBy BongoforumJanuary 14, 2026No Comments3 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Reddit Telegram Email
    NAFASI 709 za Kazi Mwalimu Daraja la IIIC Hisabati (Mathematics) Utumishi
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

    NAFASI 709 za Kazi Mwalimu Daraja la IIIC Hisabati (Mathematics) Utumishi

    MWALIMU DARAJA LA III C – HISABATI (MATHEMATICS) – Nafasi 709

    MAJUKUMU YA KAZI

    i. Kuandaa azimio la kazi, maandalio ya masomo, nukuu za masomo na Mpango wa Kazi wa majukumu mengine aliyokabidhiwa;

    ii. Kutengeneza na Kufaraghua zana za kufundishia na kujifunzia;

    iii. Kufundisha, kufanya Tathmini na kutunza kumbukumbu za Maendeleo ya Wanafunzi;

    iv. Kusimamia na kufuatilia mahudhurio ya wanafunzi Shuleni na Darasani;

    v. Kusimamia malezi ya wanafunzi Kiakili, Kimwili, Kiroho na kutoa ushauri nasaha na unasihi;

    vi. Kutoa ushauri wa Kitaalamu na kutaaluma kuhusu maendeleo ya Elimu;

    vii. Kusimamia na utunzaji wa vifaa na mali za Shule; na

    viii. Kazi nyingine atakazopangwa na Mkuu wa Shule kulingana na majukumu ya Shule.

    SIFA ZA MWOMBAJI

    Kuajiriwa mwenye Shahada ya Elimu (Bachelor with Education) au Shahada ya Ualimu (Bachelor of Education) yenye somo la kufundishia la Hisabati
    AU
    Shahada isiyo ya Ualimu/Elimu yenye somo la kufundishia la Hisabati pamoja na Stashahada ya Uzamili ya Elimu (Postgraduate Diploma in Education) kutoka Vyuo vya Elimu ya Juu vinavyotambulika na Serikali.

    NGAZI YA MSHAHARA
    TGTS- D

    MASHARTI YA JUMLA

    1. Waombaji wote lazima wawe raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wasizidi umri wa miaka 45. Hata hivyo, kwa nafasi za ndani ya Taasisi za Kijeshi: Waombaji wa nafasi zisizo za shahada wasizidi umri wa miaka 25.
    Waombaji wa nafasi za shahada wasizidi umri wa miaka 30.

    2. Waombaji wenye ulemavu wanahamasishwa kutuma maombi na wanapaswa kuainisha kwenye mfumo wa kuombea ajira ulemavu walionao kwa ajili ya taarifa kwa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.

    3. Waombaji wote waambatishe cheti cha kuzaliwa kilichothibitishwa na Mwanasheria/Wakili.

    4. Waombaji kazi ambao ni waajiriwa katika Utumishi wa Umma,WASIOMBE na wanatakiwa kuzingatia maelekezo yaliyopo katika waraka namba CAC45/257/01/D/140 wa tarehe 30 Novemba 2010.

    5. Maombi yote yaambatane na vyeti vya taaluma, maelezo, nakala za vyeti vilivyothibitishwa na Mwanasheria/Wakili ambavyo ni vyeti vya kuzaliwa, vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika:- Postgraduate/Degree/Advanced Diploma/Diploma/Certificates. Vyeti vya kitaaluma (Professional certificates from respective boards)

    6. “Testmonials”, “Provisional Results”, “Statement of results”, hati matokeo za kidato cha nne na sita (FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS) HAVITAKUBALIWA.

    7. Waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na Mamlaka husika (TCU, NECTA na NACTVET). Kwa waombaji wa kada zinazohitaji ‘GPA’ waliosoma nje ya Tanzania waambatishe cheti cha ukokotozi wa ‘GPA’ kutoka TCU.

    8. Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kama wana kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.

    9. Uwasilishaji wa taarifa na sifa za kughushi wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.

    10. Mwisho wa kutuma maombi ya kazi ni tarehe 28 Januari, 2026.

    11. Kumbuka kuambatisha barua yako ya maombi ya kazi iliyosainiwa pamoja na vyeti vya elimu, anuani ya barua hiyo ielekezwe kwa;
    KATIBU,
    OFISI YA RAIS,
    SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA,
    S. L. P. 2320,
    Mtaa wa Mahakama, Tambukareli,
    DODOMA.

    12. Maombi yote yatumwe kwenye mfumo wa kielektroniki wa Ajira (Recruitment Portal) kupitia anuani ifuatayo;https://portal.ajira.go.tz/. (Anuani hii pia inapatikana kwenye tovuti ya Sekretarieti ya Ajira kwa kuingia sehemu iliyoandikwa ‘Recruitment Portal’).

    13. Maombi yatakayowasilishwa nje ya utaratibu ulioainishwa katika tangazo hili HAYATAFIKIRIWA.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleNAFASI 912 za Kazi Utumishi (MDAs & LGAs)
    Next Article NAFASI 201 za Kazi Mwalimu Daraja la IIIC Fizikia (Physics) Utumihi
    Bongoforum
    • Website

    Related Posts

    Ajira

    MAJINA Walioitwa Kazini Taasisi Mbalimbali za Umma

    January 14, 2026
    Ajira

    NAFASI za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo

    January 14, 2026
    Ajira

    NAFASI za Kazi Manispaa ya Tabora

    January 14, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    Demo
    Top Posts

    NAFASI za Kazi Kutoka Ajira Portal January 2026

    January 12, 2026427 Views

    NAFASI 912 za Kazi Utumishi (MDAs & LGAs)

    January 14, 202631 Views

    NAFASI 142 za Kazi Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT)

    January 11, 202630 Views
    Stay In Touch
    • Facebook
    • YouTube
    • TikTok
    • WhatsApp
    • Twitter
    • Instagram
    Latest Reviews

    Subscribe to Updates

    Get the latest tech news from FooBar about tech, design and biz.

    Demo
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest
    • Home
    © 2026 BongoForum. Designed by BongoForum.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.

    Ad Blocker Enabled!
    Ad Blocker Enabled!
    Our website is made possible by displaying online advertisements to our visitors. Please support us by disabling your Ad Blocker.